Monday, 12 June 2017

MIMI MWANAWAKE NAJITAMBUAJE


MWANAMKE NI NANI

 Mwenyezi Mungu akaumba mtu kwa mfano wake(mwanzo 1:27), kwa mfano wa Mungu alimwumba,mwanaume na mwanamke aliwaumba. Sisi wanawake ni watu wenye nguvu na ushawishi mkubwa katika kufanya mambo mengi kuliko wanaume. Endapo tutafanya mambo kwa kusudi la MunguTutambue tuliumbwa wanawake si kwa bahati mbaya bali Mungu alikuwa na kusudi jema la kutuumba na kutuweka katika ulimwengu huu, kwa hiyo tuamini nafasi yetu kama wanawake ni ya Muhimu mahali popote pale,sisi ni kama chumvi, na chakula kikikosa chumvi kinakuwa akina ladhaBwana alikuwa ameumba tayari wanyama , lakini mwanaume hakuwa na mwenza,alikuwa peke yake.Katika ubavu wa mwanamme Mungu akamtolea mwanamke .Mwanaume akamtambua mwanamke kama nyama yake
Wanawake ni Furaha

Kama wanawake tusisubiri tuwezeshwe inatakiwa tujiwezeshe kwanza wenyewe, kujishughulisha katika shughuli mbalimbali ya kujiinua kiuchumi, kuwa washauri bora katika nchi , jamii na familia zetu, kama wanawake tunatakiwa tuongeze juhudi za ziada na nia ya mafanikio  katika mambo mbalimbali , Iwapo imetokea aneth au judith ameshindwa katika jambo fulani inaonekana wanawake ndo wameshindwa, hata jambo baya linapotokea akiwa amefanya mama au binti yoyote itajulikana ni mwanamke amekosea , yatupasa wanawake tuonyesha picha nzuri katika jamii yetu ili tutunzee thamani yetu.

MIMI MWANAWAKE NAJITAMBUAJE

MWANAMKE NI NANI  Mwenyezi Mungu akaumba mtu kwa mfano wake(mwanzo 1:27), kwa mfano wa Mungu alimwumba,mwanaume na mwanamke aliwaumba. ...